Kuna mirija katika jicho kwa ajili ya kupitisha machozi ili kulainisha jicho. Kutokana na sababu mbalimbali hii mirija inaweza ziba.
Kuziba kwa mirija ya machozi kunaweza sababisha kutokwa sana na machozi, pia inaweza sababisha jicho kuvimba na kuuma na kutokuona vizuri.
Kwa watoto wadogo mirija inaweza funguka yenyewe kwa kukanda sehemu husika. Wakati mwingine upasuaji huhitajika kwa ajili ya kufungua mirija ya machozi iliyoziba